HOUSE OF ENTERTAINMENT


JOIN KENYASWAHILINEWS
!-- AdsAgony - Ad Display Code -->

MPYA MPYA ZA LEO

HABARI (193) Michezo (121) BURUDANI (86)

Jumapili, 29 Aprili 2018

Pamoja na kipigo lakini Wenger apewa zawadi na Ferguson


 Kocha wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson leo amemuaga kocha wa Arsenal Arsene Wenger kwa kumpa zawadi maalum kabla ya mechi ya ligi kuu iliyomalizika kwa kufungwa 2-1 usiku huu kuanza.

Fergusona amemkabidhi zawadi hiyo kwaniaba ya klabu ya Manchester United ikiwa ni sehemu ya kutambua mambo mbalimbali ambayo Wenger ameyafanya kwenye ligi kuu ya soka ya England EPL.

Wenger ametangaza rasmi kuachana na Arsenal aliyoifundisha kwa miaka 22 mwishoni mwa msimu huu. Hata hivyo Wenger bado hajaweka wazi kama atastaafu au atakwenda kufundisha timu nyingine.

Katika mchezo uliopigwa jioni hii kwenye uwanja wa Old Trafford, Wenger ameshinwa kulinda heshima ya kutofunga baada ya vijana wake kuruhusu bao la dakika za mwisho kutoka kwa Marouane Fellaini.

Mabao ya Man United yamefungwa dakika ya 16 na kiungo Paul Pogba na dakika ya 90 na Marouane Fellaini huku lile la Arsenal likifungwa na Henrikh Mikhtaryan dakika ya 51. Wenger na Mourinho sasa wamekutana mara 13 na Mourinho ameshinda mara 8 na kutoka sare mara 5.