Hii ndio ratiba ya nusu fainali kombe la shirikisho
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewataarifu wapenzi wa soka nchini kuwa michuano ya kombe ya Shirikisho (ASFC) kwa hatua ya nusu fainali inatarajiwa kuanza kutimua vumbi mnamo Aprili 20 na 21, 2018 kwa timu nne zilizoweza kufuzu nafasi hiyo.
Hayo yamewekwa wazi na Afisa Habari wa TFF, Cliford Mario Ndimbo wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam na kusema nusu fainali ya kwanza itachezwa siku ya Ijumaa Aprili 20,2018 ikiwakutanisha Stand United ya Shinyanga watakaokuwa wenyeji wa Mtibwa Sugar ya Morogoro kwenye uwanja wa Kambarage Mkoani Shinyanga.
Aidha, Ndimbo amesema timu ya Singida United watawakaribisha JKT Tanzania kwenye nusu fainali ya pili itakayochezwa katika dimba la Namfua siku ya Jumamosi Aprili 21,2018.
Kwa upande mwingine, Ndimbo amesema washindi kwenye nusu fainali hizo watacheza mchezo wa fainali Mei 31, 2018.