Hili Povu la Mange Kimambi kwa Joketi si la Nchi Hii " Kujitoa Kote Kule Kwenye Seduce me Leo Kaolewa Mwingine?? Inachoma Kama Pasi''
Mwanadada mwanaharakati Mange Kimambi amemtolea povu si la nchi hii jokate mwegelo baada ya Alikiba kuoa mwanamke mwingine huko mombasa nchini kenya badala ya yeye ambaye alikua naye kwenye mahusiano kwa muda mrefu.
Mange ameonekana kutokuwa upande wa Joketi kwa kumuona kama msaliti katika nchi kwa kujiunga na CCM huku wananchi wakiteseka na kusema kuwa sasa laana ya usaliti inamtafuna.
Kupitia akaunti ya istagram mage aliandika Hivi ' laana za kusaliti taifa lako jojo watanzania wenzako wanauawa, wanatekwa, wanafungwa, wanaonewa, wananyanyaswa wewe ulikua ujali sababu unanufaika na utawala wake. Ndo malipo haya na bado." ila Tumemekomeshwa wote hata mimi naumia ni vile maandamano yananikeep busy la sivyo ningechamba leo. Kujitoa Kote Kule kwenye seduce me leo kaolewa mwingine?? inachoma kama pasi''
Alikiba leo amemuoa mwanamke kutoka mombasa ambapo sherehe yake kufanyika huko huko jion ya leo huku ndugu na jamaa zake wakionekana kushiriki katika tukio hilo la historia kwa Alikiba.