HOUSE OF ENTERTAINMENT


JOIN KENYASWAHILINEWS
!-- AdsAgony - Ad Display Code -->

MPYA MPYA ZA LEO

HABARI (193) Michezo (121) BURUDANI (86)

Alhamisi, 12 Aprili 2018

Ukiachana na Daimond Mimi Ndio Mwenye Mjengo Mkali Kuliko Wasanii Wote- Harmonize

Ukiachana na Daimond Mimi Ndio Mwenye Mjengo Mkali Kuliko Wasanii Wote- Harmonize

Msanii wa muziki kutoka label ya WCB, Harmonize amefunguka kuhusu mjengo wake ambao upo mbioni kukamilika.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma ‘Kwa Ngwaru’ ameiambia Funiko Base, Radio Five kuwa mjengo huo upo mbioni kumalizika na utamfanya kuwa msanii wa pili Bongo kuwa na nyumba kali.

“Nasema ukweli mimi nyumba yangu ikiisha, nyumba ninayojenga mimi sijui nitakuwa msanii wa pili wa Dar es Salaam au Tanzania kuwa na nyumba kali, ya kwanza ni Diamond ambayo nayo haijaisha ila ipo katika hatua za mwisho,” amesema Harmonize.

Ameongeza kuwa amefikia mafanikio hayo makubwa kutokana na ushauri mzuri anaopatiwa na mpenzi wake Sarah.

Katika hatua nyingine amefunguka tetesi za mpenzi wake Sarah kuwa na ujauzito na kueleza kuwa hilo halina ukweli ila kwa sasa anaweka mazingira mazuri kwa ajili ya mtoto.