HOUSE OF ENTERTAINMENT


JOIN KENYASWAHILINEWS
!-- AdsAgony - Ad Display Code -->

MPYA MPYA ZA LEO

HABARI (193) Michezo (121) BURUDANI (86)

Jumanne, 1 Mei 2018

Barua ya wazi kwa Askofu Fred Shoo


jamiiforums.com

Salam katika jina la bwana wetu Yesu Kristo.

Kwa mara ya kwanza kanisa letu linapitia ugumu kutokana na mtindo wako wa mkono wa chuma na ubinafsi wa maoni na fikra.

Baba askofu kanisa ni chombo "laini" (delicate) hivyo kuwa makini kwani waumini wana mitazamo yao na mararajio kutoka katika kanisa lao.

Usiturudishe tuliko toka hasa sisi waumini wa DMP kwani ilituchukua takribani miaka kadhaa ya mgogoro enzi za Jerry Mngwamba hadi kumpata Dr.Malasusa ambaye kwa kiwango kikubwa katuunganisha wana DMP.

Zama hizo za akina Jerry Mngwamba wewe ulikuwa bado upo Uswaaa,Machame.Tunajua huna cha kupoteza zaidi ya kupigania maslahi yako kuwafurasha rafiki zako.

Kuna mambo mengi binafsi unayafanya na kuamua na kisha kujificha kwenye kivuli cha baraza la maaskofu.

Hakika muda unafika na hayo yote unayoyafanya kulibomoa kanisa yatakurudia kwa mtindo wa karma.

Wito wangu kwako ni ujirekebishe kwani muda bado.Siku zote hila mbaya haidumu kwani hudhihirika.Pia jitahidi kuficha hisia zako kisiasa kutokana na nafasi yako kwani utadharaulika na utajuta.

Askofu Shoo lolote ovu dhidi ya Malasusa na DMP halitafanikiwa na mtaumbuka kama wajenzi wa mnara wa babeli.DMP ni kioo cha KKKT hivyo hatutaruhusu wahuni kutaka kuibadilisha DMP kama genge lao kupiga soga.

Mungu ndiye mtetezi wa DMP dhidi ya wote wenye nia ya kutuvuruga na kuibadilisha iwe Chama cha siasa.

Tunamkabidhi MUNGU ole kwao wenye nia ovu.