HOUSE OF ENTERTAINMENT


JOIN KENYASWAHILINEWS
!-- AdsAgony - Ad Display Code -->

MPYA MPYA ZA LEO

HABARI (193) Michezo (121) BURUDANI (86)

Jumapili, 20 Mei 2018

CHELSEA MABINGWA FA 2017/18


Chelsea imetawazwa mabingwa wapya wa kombe la FA baada ya kuifunga Manchester United bao moja katika mchezo wa fainali uliofanyika uwanja wa Wembley.

Bao pekee kwenye mchezo huo lilifungwa na Eden Hazard kwa mkwaju wa penati dakika ya 22 baada ya kufanyiwa madhambi ndani ya 18 na mlinzi Phil Jones.

United ilimiliki sehemu kubwa ya mchezo huo ikifanya mashambulizi mengi langoni mwa Chelsea lakini hawakufanikiwa kupata bao la kusawazisha.
Chelsea walifanya mashambulizi machache ya kushtukiza wakitumia mipira mirefu wakimtumia Hazard na Oliver Giroud walio ongoza safu ya ushambuliaji.

Arsenal ndio walikuwa mabingwa watetezi wa michuano hiyo baada ya kuifunga Chelsea mabao 2-1.