globalpublishers.co.tz
PRESHA ya mchezo inaweza kukufanya ukafanya maamuzi ambayo ni magumu, ndivyo ilivyokuwa baada ya nahodha wa Yanga, Kelvin Yondani kuonekana akizuia mabadiliko ya kumtoa kiungo, Papy Tshishimbi katika mchezo wa jana dhidi ya Simba.
Tukio hilo lilitokea kipindi cha pili baada ya Simba kuwa mbele kwa bao 1-0 huku Yanga wakiwa pungufu kutokana na beki Hassan Kessy kupewa kadi nyekundu, ndipo benchi la ufundi likawa linataka kumtoa Tshishimbi lakini Yondani akaelekea kwenye benchi na kuonekana akitoa ushauri wa kutofanya hivyo.
Licha ya ushauri huo bado Tshishimbi alitolewa katika dakika ya 80 na nafasi yake kuchukuliwa na Emmanuel Martin lakini hiyo haikuchangia kubadilisha matokeo ya mchezo huo ambapo Simba ilishinda bao 1-0.