Mwanamuziki mahiri wa Bongofleva nchini Ali Kiba, leo amefunga ndoa na Binti wa Kimombasa ajulikanae kwa jina la Bi.Amina Khalef,ndoa hiyo imefungwa katika msikiti wa Ummu Kulthum uliopo mjini Mombasa nchini Kenya,ambapo hafla hiyo imehudhuriwa na watu wa aina mbalimbali wakiwemo mashuhuri .Aidha taarifa zinaeleza kuwa Harusi hiyo itakayokuwa ya aina yake itarushwa LIVE na kituo cha televisheni ya AZAM jioni ya leo.
Mwanamuziki mahiri wa Bongofleva nchini Ali Kiba akizungumza na 'mpambe' wake leo wakati akifunga ndoa na Binti wa Kimombasa ajulikanae kwa jina la Bi.Amina Khalef,ndoa hiyo imefungwa katika msikiti wa Ummu Kulthum uliopo mjini Mombasa nchini Kenya.
Alikiba akifurahia jambo na marafiki zake mara baada kufunga ndoa
Ali Kiba akifurahia jambo akiwa na ndugu,jamaa na marafiki zake waliomsindikiza kwenye kuchukua 'jiko' mapema leo asubuhi huko mjini Mombasa.
Msanii alikiba na Wapambe wake wakielekea kufunga ndoa.




