MWANAUME ANAYETUHUMIWA KUMUUA RADIO,MAPYA TENA YAJIRI
Ni miezi miwili imepita tokea marehemu Radio afariki February 1, 2018, Radio ambae alikuwa pamoja na Weasel wakiunda kundi la Goodlyfe kutokea nchini Uganda, msiba wa Radio uligusa watu wengi duniani. Baada ya Radio kufariki mtuhumiwa
Wamala Godfrey alias Troy anayedaiwa kusababisha kifo cha Radio alikimbia na hakuonekana kwa wiki kadhaa lakini baada ya polisi kuendesha msako wa walifanikiwa kumkamata. Wamala Godfrey alias Troy amekiri kuwa alisababisha kifo cha Radio na kusema kuwa
Radio alimponyoka mikononi mwake na kujipigiza kichwa chake chini wakiwa wanapigana haikuwa lengo lake kumuua na hivyo kuomba msamaha ila hadi sasa mtuhumiwa anashikiliwa na polisi kutokana na mauaji aliyoyasababisha.