Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewaasa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini kuacha tabia ya kufanya siasa wanapokuWa chuoni bali watumie muda mwingi kusoma na kufanya tafiti mbalimbali kwa ajili ya kusaidia wananchi wa Tanzania.

Rais Magufuli amesema hayo leo Mei 07 2018 wakati wa ziara katika chuo cha kilimo (SUA) Mkoani Mororgoro ambapo amesema kuwa serikali inatoa fedha nyingi sana kuwapa mikopo wanafunzi wa elimu ya juu na kuongeza kuwa hatasita kuchukua hatua.
“Niwaombe wanachuo mpo hapa kwa ajii ya shule, tekelezeni wajibu wenu, msipoteze muda wenu katika masuala yasiyokuwa na tija, tumewapa mkopo watu 6600 nitasikitika sana kama hii mikopo kutoka kwa wananchi masikini, mfanye manbo ambayo hayaendani na yale ambayo mmeletwa kufanya, msivigeuze vyuo maeneo ya kufanya siasa” alisema Magufuli
Rais Dkt. Magufuli alisema kuwa serikali yake haitasita kuchukua hatua ikiwemo kuawafukuza chuo wanafunzi ambao watakuwa kinara wa kusababisha migomo na kuongeza kuwa wengi wao ni wale ambao wanakua na matokeo mabaya ya kitaaluma.
Awali Rais Magufuli alipongeza uongozi wa chuo hicho kwa kufanikiwa kutekeleza miradi mbalimbali ya utafiti, kilimo na ufugaji na kuahidi kutoa kiasi cha shilingi bilioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa mabweni chuoni hapo.