HOUSE OF ENTERTAINMENT


JOIN KENYASWAHILINEWS
!-- AdsAgony - Ad Display Code -->

MPYA MPYA ZA LEO

HABARI (193) Michezo (121) BURUDANI (86)

Jumatano, 2 Mei 2018

Rais JPM Ahoji Jambo Hili " Kwani Kusoma ndo Kujua Kingereza


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.John Pombe Magufuli amehoji wanafunzi wa chuo cha Mkwawa kwamba kujua kusoma ni kujua Kiingereza.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo, Mei 2 wakati akizungumza na wanafunzi pamoja na wafanyakazi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa, kilichopo mkoani Iringa wakati akitoa ufafanuzi wa shule za private na shule za Sekondari.

“Eti mtu amemaliza form 4 hajui kuandika barua ya kingereza. Kwani kusoma ni kujua kingereza? Wachina wanajua kingereza? mbona wanatengeneza mashine,” amehoji Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amesema kuwa “Shule za private wanafunzi wake wanachujwa, wakifika form 2 kuingia form 3 wanawachuja tena. Wanabaki na ile cream ili waonekane wanaongoza. Serikali inayowapenda wananchi wake haiwezi ikafanya hivyo.”