HOUSE OF ENTERTAINMENT


JOIN KENYASWAHILINEWS
!-- AdsAgony - Ad Display Code -->

MPYA MPYA ZA LEO

HABARI (193) Michezo (121) BURUDANI (86)

Jumanne, 8 Mei 2018

Yanga kutumia kikosi B mech za ligi kuu

Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ameshauri uongozi kupeleka kikosi cha timu ya vijana, maarufu kama Yanga B katika mechi zake mbili za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons mjini Mbeya na Mtibwa Sugar mjini Morogoro, ili kikosi cha kwanza kiendelee na maandalizi ya mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Rayon Sport ya Rwanda Jumatano ijayo.

Zahera amesema kwa sasa Yanga wanapaswa kuelekeza nguvu zao kwenye mechi za Kombe la Shirikisho la Soka Afrika baada ya kupoteza nafasi ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu.

Zahera ameyasema hayo leo mchana Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam wakati kikosi cha Yanga kikiwasili kutoka Algiers nchini Angeria ambako Jumapili kilifungwa mabao 4-0 na wenyeji, U.S.M. Alger katika mchezo wake wa kwanza wa Kundi D Kombe la Shirikisho Uwanja wa Julai 5, 1962.

“Hatuna nafasi kwenye ligi, hivyo tunatakiwa kuweka nguvu zote kwenye kombe la Shirikisho, nimewaomba viongozi wapeleke kikosi B katika michezo yetu ya ligi, ili nibaki na kikosi cha kwanzaa nikiandae kwa ajii ya mchezo dhidi ya Rayon”.

"Tunatakiwa kujiandaa vema ili tusipoteze mchezo huo, ukiangalia ratiba ya ligi imekaa vibaya kwetu, tumefika leo, kesho tunatakiwa kwenda Mbeya, baadaye tuna mchezo Morogoro, kabla ya kuivaa Rayon, ndio maana nimewaomba wakubwa tuwaze zaidi kombe la Shirikisho,”amesema.

Akizungumzia kipigo cha Algeria, Zahera alisema kikosi chake kiipoteza mchezo huo kutokana na kukosa wachezaji wazoefu.

“Tulipoteza mchezo kwa kukosa uzoefu, hatukuwa na wachezaji wetu wazoefu, hivyo uwanjani tulikuwa na watoto watano, wenzetu walitumia mwanya huo kutuadhibu. 

"Kwenye mpira uzoefu ni jambo la msingi, vijana walijitahidi kucheza kwenye majukumu waliyopewa, lakini walikosa umakini,”alisema.