HOUSE OF ENTERTAINMENT


JOIN KENYASWAHILINEWS
!-- AdsAgony - Ad Display Code -->

MPYA MPYA ZA LEO

HABARI (193) Michezo (121) BURUDANI (86)

Jumatatu, 9 Aprili 2018

Uongozi wa Azam waitupia lawama Mbeya city

Uongozi wa Azam waitupia lawama Mbeya city
Baada ya mchezo wa ligi kati ya Mbeya City na Azam FC kwenda suluhu ya bila kufungana katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, uongozi wa Azam waitupiwa lawama Mbeya City.
Kupitia Afisa Habari wa Azam, Jaffer Idd Maganga, alisema kuwa wachezaji wa Mbeya hawakuwa wanacheza mpira kupata matokeo bali walipambania pointi moja.
Maganga alieleza kuwa wapinzani wao walikuwa wanatumia muda mwingi kupoteza muda huku akieleza kuwa walikuwa wameridhika ilihali wao walikuwa wanapambana kujipatia alama 3 muhimu.
Azam iliambulia alama moja kwenye mchezo na kuzidi kusalia katika nafasi ya 3 ya msimamo wa ligi kuu bara ikiwa na pointi 45 huku ikicheza jumla ya michezo 23 mpaka sasa.