HOUSE OF ENTERTAINMENT


JOIN KENYASWAHILINEWS
!-- AdsAgony - Ad Display Code -->

MPYA MPYA ZA LEO

HABARI (193) Michezo (121) BURUDANI (86)

Jumapili, 8 Aprili 2018

Siri ya Okwi na Bocco VPL

SIMBA wana mzuka kwelikweli kusaka ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu, lakini kuna siri kubwa imejificha ndani yake kuhusiana na kasi ya upachikaji mabao ya straika wake, John Bocco.

Bocco ameshafunga mabao 12 mpaka sasa huku kasi yake ikizidi kuwa moto na tayari ametoa onyo kwamba, anataka kumalizika msimu akiwa na Kiatu cha Dhahabu.

Lakini, nyuma ya mafanikio ya Simba na Bocco sambamba na kinara wa mabao wa Ligi Kuu Bara na staa wa Simba, Emmanuel Okwi (16), kuna fundi mmoja anaitwa Shomary Kapombe, ambaye ndiye mpango mzima.

Kuna siri kubwa imejificha kati ya Kapombe, Okwi na Bocco wakilenga kuhakikisha iwe jua au mvua ubingwa msimu huu unatua Msimbazi sambamba na tuzo ya mfugaji bora ili kukata kiu ya mashabiki.

Sasa iko hivi, Kapombe amefichua kuwa wakati akiwa majeruhi kabla ya kurejea uwanjani, waliketi na Bocco na kupanga mikakati ya kutengeneza nafasi nyingi za kufunga ili kufikia malengo.

Katika kutekeleza maazimio hayo, Kapombe alirejea kwa mara ya kwanza kwenye mchezo dhidi ya Kagera Sugar na akatengeneza nafasi ya bao la pili kwa Bocco.

“Tuna makubaliano na Bocco na Okwi kuhakikisha tunatimiza malengo msimu huu, tunataka ubingwa na tuzo za kutosha ikiwemo Kiatu cha Dhahabu.

“Kuna mechi tisa zimebaki ambazo natakiwa kutengeneza nafasi za mabao za kutosha kwa Bocco ili afikie mabao idadi ya magoli 15 ambayo yanatosha kwa msimu huu wa kwanza na si mbaya akifunga zaidi,” alisema Kapombe.

“Wakati nahangaika na Bocco, pia nina kazi kama hiyo kwa Okwi ambaye anataka kufunga mabao yasiyopungua 20 msimu huu. Kwa kufanya hivyo tutachukua ubingwa na tuzo ya ufungaji na hata mchezaji bora wa kigeni,” alisema.